This is humanly impossible. Another World Record 1 mile 4:07:64 Faith is on her own Level.
#jomo #DiamondLeague #faithkipyegon #babuowino #uhuru #Demonstrations #TV47Wikendi
Gavana wa Kilifi Gideon Mung'aro alilazimika kubadili mawazo yake kuhusu tishio lake la kuondoa na kusafirisha miili ya wahasiriwa wa shakahola ambazo zimehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha hospitali ya kaunti ndogo ya Malindi hadi Nairobi.
#TV47Wikendi
Wakati shule zinajiandaa nchini kufunguliwa kwa muhula wa pili kesho, hali katika baadhi shule kaunti ya Homa Bay ni mbaya. Familia zilizopiga kambi katika shule kutokana na athari za mafuriko zikianza kuhamishwa hadi kanisani ili kutoa nafasi kwa ufunguzi wa shule.
#TV47Wikendi
Baada ya Rais William Ruto kuliongoza taifa katika upanzi wa miche siku ya ijumaa katika msitu wa kiambicho kaunti ya Murang'a, kampeni ya upanzi wa miti bilioni 15 ifikiapo mwaka wa 2032. Wizara ya mazingira imetoa ratiba ya kuongoza shughuli hiyo ya kila mwezi.
#TV47Wikendi
SOLEMBA YA MADAKTARI WAKUFUNZI?
Mgomo wa madaktari umemalizika siku ya 59.
Madaktari wanagenzi wanahisi wamesalitiwa na KMPDU
Madaktari wanagenzi watakaa nyumbani kwa miezi miwili ya ziada.
Paul Kirobi
#TV47Wikendi
Mswada wa fedha wa 2024, unaopendekeza ushuru zaidi kwa bidhaa na huduma muhimu kama njia ya kutafuta mapato zaidi ya kukwamua uchumi wa taifa sasa umeibua hisia miongoni mwa viongozi pamoja na wakenya.
#TV47Wikendi #mothersday2024
Andrine Kilemi
AFC Leopards wamenadikisha ushindi wa bao moja kwa sufuri dhidi ya Bandari kwenye mechi ya raundi ya 18 ya ligi kuu ya soka nchini Kenya.
#TV47Wikendi
Andrine Kilemi
Mkongani Boys na Kachochoroni Girls wamejikatia tiketi ya kushiriki kwenye fainali ya kitaifa ya dimba la Europe Day baada ya kutwaa ubingwa.
#TV47Wikendi
Andrine Kilemi
Idara ya utabiri wa hali ya hewa nchini imetoa tahadhari kuhusu mvua kubwa inayoendelea, hususan mwezi wa mei, ambayo inaadhiri Nairobi, Pwani, Bonde la ufa, na maeneo ya Nyanza.
#TV47Wikendi
Andrine Kilemi
Muungano wa wauguzi nchini kenya umetishia kujiunga na mgomo wa madaktari ambao umekumba taifa kwa zaidi ya siku 50 kwa sasa ikiwa serikali haitazingatia masharti yao ya kuhudumu.
#TV47Wikendi
Andrine Kilemi
Wadadisi sasa wanasema, msimu wa tohara katika jamii za Sabaot, Bukusu na Batura katika kaunti ya Bungoma huchangia pakubwa ongezeko la visa vya mimba za mapema na hata dhuluma za kijinsia.
#TV47Wikendi
Andrine Kilemi
Wakati mafuriko yanayoendelea kuleta uharibifu na hasara nchini hasa katika kaunti ya Homa Bay, mgogoro mpya unatokea wakati wasiwasi unapoongezeka kuhusu usalama wa mtoto wa kike, ambaye sasa anakabiliwa na hatari kubwa ya unyanyasaji wa kijinsia.
#TV47Wikendi
Andrine Kilemi
Waathiriwa wa mkasa wa mafuriko eneo la Mai Mahiu katika kaunti ya Nakuru wameanza kuhamishwa rasmi leo kwenye nyumba za kukodisha kwa wale waliokuwa wamekodi awali, na kwa makao ya muda kwa wale walio na ardhi humo.
#TV47Wikendi
Andrine Kilemi
MATAYARISHO YA LIONESSES
Timu ya taifa ya Lionesses imekita kambi ugani Kasarani
Lionesses inajiandaa kwa michuano ya kufuzu kwa Olimpiki
Kikosi hiki kutashindana nchini Poland na Uhispania
Paul Kirobi
#TV47wikendi
MZOZO WA SHAMBA KAREN
Vurugu ilitokea kwenye barabara kuu ya Southern bypass
katika eneo ya Mamba village mtaani Karen
Kufuatia mzozo wa kipande cha ardhi takriban ekari 66
Paul Kirobi
#TV47Wikendi
Kila jumapili ya pili mwezi mei ulimwengu huadhimisha siku ya akina mama, hapa nchini wakenya wametumia fursa hii kuwapongeza mama mzazi na wale waliochukua majukumu ya kuwa walezi wao. Sherehe hii ilifungua mwanya wa biashara kwa wengine.
#TV47Wikendi #mothersday2024
HASARA YA BOMOA BOMOA KANDUYI
Watu wawili waokolewa kutoka jengo lililoporomoka Bungoma
Sehemu ya jengo hili ilikua imebomolewa na serikali ya Kaunti
Wakazi wanataka sehemu zilizobomolewa kulindwa
Paul Kirobi
#TV47Wikendi
Kituo cha kudhibiti majanga nchini – NDOC kimekanusha madai kwamba bomoa bomoa inayoendelea inalenga wakenya wanaoishi mitaa ya mabanda jijini Nairobi.
#TV47Wikendi #mothersday2024
Andrine Kilemi
Serikali imetangaza kuwa nguvu za kimbunga Hidaya zimekwisha kwenye pwani ya Kenya. Idara ya utabiri wa hali ya anga imesema hayo mapema leo. Hayo yakiarifiwa, mvua nyingi inatarajiwa kuendelea kunyesha katika kaunti 37.
#TV47Wikendi
Andrine Kilemi George Maringa