KYIV, Ukraine - Ofisi ya Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy imesema kuwa kiongozi huyo amesitisha ziara zake zote za nje ya nchi zilizokuwa zimepangwa kufanyika kutokana na mashambulizi mapya ya Urusi.
#HabarileoUPDATES
DODOMA - Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa leo Mei 16, 2024 amefanya mazungumzo na Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IJP) Camillus Wambura, Ofisini kwa Waziri Mkuu Bungeni jijini Dodoma.
Picha na OWM
#HabarileoUPDATES
IRINGA - SERIKALI imetoa tahadhari dhidi ya dawa zinazotembezwa mkononi ikiwa ni pamoja na zinazouzwa katika vyombo vya usafiri kinyume na sheria ikitaja dawa nyingi ni duni na bandia.
#HabarileoUPDATES
NYANG’HWALE, Geita - KAMANDA wa Polisi mkoa wa Geita, Safia Jongo amepiga marufuku serikali za vijiji pamoja na polisi jamii kupitisha azimio la kuwafukuza watuhumiwa wa uhalifu kwenye maeneo yao badala yake wafuate sheria.
#HabarileoUPDATES
Hotuba ya Bajeti ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari
Leo Mei 16, 2024
scan 👇kufuatilia hotuba mbashara
#HabarileoUPDATES
DODOMA - Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akimsikiliza Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Magazeti (TSN), Asha Dachi wakati alipotembelea banda la TSN kwenye maonesho ya Taasisi na Wadau wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari mjini Dodoma.
#HabarileoUPDATES
DAR ES SALAAM - Mtangazaji mkongwe wa vipindi wa michezo katika Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Sued Mwinyi amefariki Dunia leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa TBC, Dk. Ayub Rioba Chacha amethibitisha.
#HabarileoUPDATES
Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Miundombinu Seleman Kakoso akimsikiliza Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Magazeti (TSN), Asha Dachi wakati alipotembelea banda la TSN kwenye maonesho ya Taasisi na Wadau wa Wizara ya Habari.
#HabarileoUPDATES
DODOMA - Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni amesema Wizara yake inatarajia kuajiri watumishi 4,857 katika mwaka wa fedha 2024/25 ili kuendelea kuimarisha usalama wa watu na mali zao.
#HabarileoUPDATES
SLOVAKIA - Waziri Mkuu wa Slovakia Robert Fico yuko “mahututi' hospitalini baada ya kushambuliwa kwa kupigwa risasi tano kwa kile ofisi yake imekiita 'jaribio la mauaji.'
#HabarileoUPDATES
DAR ES SALAAM - Mkurugenzi wa Huduma za Redio katika Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Aisha Dachi ameteuliwa kuwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN).
#HabarileoUPDATES
MOROGORO - Polisi mkoani Morogoro imewatia mbaroni madereva 10 kwa tuhuma za makosa ya usalama barabarani akiwemo dereva wa Lori, Samsoni Uwiringiyimana (35), raia wa Rwanda anayetuhumiwa kusababisha ajali iliyoua watu saba na kujeruhi wengine sita.
#HabarileoUPDATES
UNGUJA, Zanzibar - Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Hussein Ali Mwinyi amefungua kongamano la sita la usafiri wa anga kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki akisema kuna hatua kubwa zimefikiwa katika kukusa sekta hiyo ndogo ya usafirishaji.
#HabarileoUPDATES
BEIJING, China - Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki January Makamba amewasili jijini Beijing, China kwa ziara ya kikazi.
#HabarileoUPDATES
DODOMA - Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI Mohamed Mchengerwa amekutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa Tume ya Utumishi wa Walimu na kuelekeza Tume hiyo kuhakikisha inashughulikia kwa haraka na kikamilifu changamoto mbalimbali zinazowakabili walimu.
#HabarileoUPDATES
DODOMA - Waziri wa Maji, Juma Aweso amesema Taasisi na Mamlaka nyingine za maji sasa zitajifunza katika Mamlaka ya Maji Tanga ambayo imefanikiwa kuorodhesha Hatifungani ya Tanga UWASA katika soko la Hisa la Dar es Salaam.
#HabarileoUPDATES
DODOMA - Serikali imesema inakusudia kununua magari 265 ikihusisha magari 147 ya Makamanda wa Polisi wa Mikoa na Wakuu wa Polisi wa Wilaya zote kote nchini, Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni amesema bungeni mjini Dodoma.
#HabarileoUPDATES
Police Force TZ
NEW CALEDONIA, Ufaransa - Ufaransa imetangaza hali ya hatari na kupiga marufuku matumizi ya mtandao wa kijamii wa TikTok katika eneo lilokumbwa na ghasia la New Caledonia tangu Jumatatu.
#HabarileoUPDATES
ZANZIBAR - Tume Huru ya Uchaguzi nchini imetangaza kuwa itaanza kuboresha Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Julai Mosi mwaka huu ambapo idadi ya wapiga kura kwa uchaguzi mkuu ujao inakadiriwa kufikia 34,746,638.
#HabarileoUPDATES
DODOMA - Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Mwigulu Nchemba, bungeni jijini Dodoma, Mei 15, 2024
Picha na OWM
#HabarileoUPDATES