Naungana na Mhe Muhammad Mchengerwa, Waziri wa Maliasili na Utalii, kutoa pole zangu kwa wafiwa na watumishi wa wizara kwa kuwapoteza hao ndugu zetu. Mwenyezi Mungu awape subira katika kipindi hiki kigumu. Wapumzike kwa amani. #KSK_Balozi
Alisema Imam mmoja: Wakati unawahubiri waumini, usisahau kuihubiri nafsi yako pia.
#KSK_Balozi
Kila sekunde maishani mwetu inaumuhimu wa kipekee. Dakika, saa, siku, huanzia kwenye sekunde.
#KSK_Balozi
Tumewahi kusema katika nyakati tofauti, mfumo wa utendaji biashara nchini hauridhishi. Nilitegemea Wizara ya Fedha na Bunge watuongoze. TRA ni ile ile, sheria ni zile zile, watendaji ni wale wale. Tusiwe wavivu. Bilakupitia hizi sheria, kazi yetu itabaki kuwa ngumu. #KSK_Balozi
Kama tunaogopa kifo basi tuogope maisha zaidi. Kama kifo cha hitaji maandalizi, maisha yahitaji maandalizi makubwa zaidi.
#KSK_Balozi
USIZUNGUMZIE Pesa Zako Mbele Ya Masikini;Afya Yako Mbele Ya Mgonjwa;Nguvu Yako Mbele Ya Mnyonge; Furaha Yako Mbele Ya Mwenye Huzuni;Uhuru Wako Mbele Ya Mfungwa;Mtoto Wako Mbele Ya Mgumba; Wazazi Wako Mbele Ya Yatima. Usiwazidishie Maumivu. ✍ #KskBalozi
Alinena mzee mmoja, mwanaadam angepiga hatua kubwa maishani mwake kama angalikubali kubali kujifunza kutokana na makosa yake badala kufanya kila jitihada za kuyakanusha makosa yale.
#KSK_Balozi