Kitakachosemwa katika mkutano wa Kamukunji kitabadilisha sura ya siasa nchini: Opiyo Wandai #Maandamano #NTVAdhuhuri
Siku Ya Wahandisi Wanawake:
Wanawake wahandisi wamewaomba washikadau katika taasisi za uhandisi nchini kuwashika mkono ili kusaidia kuongeza idadi ya wanawake katika taaluma ya uhandisi. #NTVAdhuhuri
KRA limejitokeza kumdai mshonaji wa nguo katika eneo la Kapenguria malimbikizi ya ushuru wa shilingi milioni 1.74. #NTVAdhuhuri
Pembe Za Ndovu Zapatikana:
Polisi wamefanikiwa kunasa wawindaji haramu na pembe 12 za ndovu zinazoshukiwa kuuwawa katika maeneo ya Samburu na kufichwa eneo la Churo wakitafutia soko. #NTVAdhuhuri
Fedha Za Kuwatunza Wazee:
Naibu Rais Rigathi Gachagua anasema kuwa serikali imewachilia KES 16 bilioni, pesa za wanaoishi katika mazingira magumu nchini; kuwakinga kwa hali hii kupitia mpango wa inua jamii. #NTVAdhuhuri
Harufu Ya Mgomo Wa Madiwani:
Loise Wangui anaeleza shughuli za kaunti zitakazokwama iwapo madiwani watagoma. #NTVAdhuhuri
Siafu Wa KES 300,000 Waibwa:
Watu watatu wameshtakiwa katika mahakama ya uwanja wa ndege ya JKIA kwa kosa la kusafirisha wanyamapori ambao ni siafu bila kibali cha shirika la wanyama pori. #NTVAdhuhuri
Malala Amkashifu Raila:
Katibu mkuu wa chama cha UDA Cleophas Malala ameusuta mrengo wa azimio akitoa onyo dhidi ya #Maandamano kutokea. #NTVAdhuhuri
WAZIRI EZEKIEL Machogu anapendekeza gredi za kujiunga na Chuo Kikuu cha Garissa kushushwa kiasi ili kuwezesha wenyeji zaidi wanaotaka kujiunga na taaluma ya ualimu kupata elimu hiyo. #NTVAdhuhuri
Mgomo Wa Sekta Ya Matatu:
Wahudumu wa matatu watishia kugoma kote nchini iwapo NTSA haitasitisha msako unaondelea barabarani.
Waandai NTSA na polisi wanatumia msako huo kuitisha hongo.
#NTVAdhuhuri
FAMILIA YA msichana wa kidato cha pili ambaye anadaiwa kunajisiwa kinyume na ripoti ya daktari, sasa imetoa kilio kwa serikali kuingilia kati baaada ya mshukiwa kuachiliwa kwa dhamana. #NTVAdhuhuri
Huu Ni Uchungu Wa Mama?
Mwanamke achoma nyumba na kuwaua wanawe wawili Kajiado baada ya mumewe kuoa mke wa pili.
#NTVAdhuhuri Lofty Matambo Kitindamimba
Timu Ya Olimpiki Maalum:
Timu ya Kenya iliyowakilisha taifa Ujerumani yapewa makaribisho katika makaazi ya Naibu Rais Rogathi gachagua.
#NTVAdhuhuri Lofty Matambo Hillary Anekea
Azimio Ina Mpango Upi?
Raila Odinga anatarajiwa kuongoza mkutano na wafuasi wa chama hicho katika uwanja wa Kamukunji; anatarijiwa kutua nchini kutoka Poland.
Melita Oletenges #NTVAdhuhuri #Maandamano
Chonjo Kwa Siku Ya Kiswahili:
Washikadau na wapenzi wa lugha ya Kiswahili wajitokeza kutangaza makaribisho ya kushereheka siku ya Kiswahili duniani.
#NTVAdhuhuri Lofty Matambo